Mwasiti Almasi
Mwasiti alisema kuwa sababu kubwa ya wimbo huo kutopokelewa vizuri
Dar es Salaam ni mazoea ya baadhi ya mashabiki kuona msanii akifanya
vitu vyake bila kubadilika.
"Katika wimbo wa Sema Naye nimeimba tofauti na vile ambavyo
mashabiki wamezoea na hilo ni jambo la kawaida kwa msanii anayejua kile
anachokifanya, lakini bahati wachache hawakunielewa," alisema Mwasiti.
Msanii huyo aliiambia Nipashe kuwa mashabiki wamezoea kumsikia
akiimba muziki wa kizazi kipya kwa mtindo mmoja, lakini katika wimbo
wake mpya amefanya vitu vyake vipya ambavyo vimeonekana kuwa vigeni
kwao.
Hiyo ndio sababu kubwa ambayo ninaweza kusema kuwa imefanya hapa
Dar es Salaam nikutane na changamoto za wimbo wangu kutopokelewa vizuri,
lakini bahati nzuri unasikika sana mikoani," alisema.
Mwasiti ni miongoni wasanii nyota walioibuliwa na Nyumba ya Vipaji
nchini (THT) na amekuwa akifanya vizuri kwenye nyimbo zake mbalimbali
zilizomfanya awe na jina katika muziki wa kizazi kipya.
Post a Comment