0

Kundi la Muziki wa taarabu Mashauzi Classic
 
 Kundi la Muziki wa taarabu Mashauzi Classic leo linashuka kwenye Ukumbi wa  Mango Garden, Kinondoni kufanya shoo ya pamoja na Bendi ya Twanga Pepeta.
Meneja wa Mashauzi Classic, Ismail Rashid maarufu kama Suma alisema jana kuwa Kundi la Mashauzi Classic lilitua jana kutoka Muscat, Oman lililokwenda kwa ajili ya kufanya maonyesho kadhaa.
Suma alisema, itakuwa mara ya kwanza kwa bendi hizo mbili kupiga pamoja katika ukumbi huo wa Mango Garden.
Alisema Isha Mashauzi pia atatambulisha nyimbo wake mpya zijulikanayo kama “Kismat” na “Jiamini”.
 
Pia ameahidi kupiga nyimbo zake zote maarufu na zinazopendwa na mashabiki wa taarabu nchini, zikiwamo “Sura Surambi” na “Nimpe Nani”.
 
Naye mratibu wa onyesho hilo, Joseph Kapinga alisema katika mpambano huo, Twanga Pepeta watatambulisha nyimbo zao mpya kama 'Mtu Makini' utunzi wa rapa Fagason na 'Twanga Kwanza' utunzi wake Roggart Hegga Katapila.
Alisema pia Fugason ataendeleza kutambulisha rapu yake mpya ijulikanayo kama “Banjuka”.
 
Pia bendi hiyo pia itawatambulisha wanenguaji wake wapya Kama Super K na Chiku Kasika.
 
Onyesho hilo limeandaliwa na Keen Arts na Bob Entertainment chini ya udhamini wa Konyagi, LeteRaha, Fredito Entertainment, Saluti5 na CXC Africa.
 

Post a Comment

 
Top