Wajenzi wa viwanja vya kombe la dunia Qatar
Kundi la haki za
kibinadamu Amnesty International limeishtumu Qatar kwa kuwafanyisha watu
kazi kwa lazima katika uwanja utakaochezewa mechi ya ufunguzi wa
michuano ya Kombe la Dunia 2022.
Qatar imesema kuwa ina wasiwasi kuhusu madai hayo na kwamba itayachunguza.
Serikali ilisema kuwa maslahi ya wafanyikazi wahamiaji yanapewa kipaumbele na kusisitiza kuhusu marekebisho ya sheria za kazi nchini humo.
Lakini Amnesti imeonya kwamba marekebisho hayo hayataleta tofauti yoyote na kusema kwamba baadhi ya wafanyikazi ''wanakabiliwa na wakati mgumu''.
Post a Comment