Watu
 tisa (9) wamejeruhiwa katika vurugu wakati wa kuwaondoa wafanyabiashara
 wadogowadogo sehemu zisizo ruhusiwa wilayani Nyamagana, mkoani Mwanza
Taarifa
 ya Kamanda wa Polisi Mkoa w Mwanza DCP Ahmed Msangi imesema kwamba 
tukio hilo limetokea mnamo tarehe 05.03.2017 majira ya saa15:45hrs 
katika mtaa wa Buhongwa Center ambapo watu tisa wakiwemo askari mgambo 
wa jiji la mwanza saba (07), afisa mazingira mmoja (01) na dereva wa 
jiji mmoja (01) walijeruhiwa.
Amesema
 watu hao walijeruhiwa kwa kupigwa na mawe sehemu mbalimbali ya miili 
yao na wafanyabiashara wadogowadogo waliokuwa wakifanya biashara pembeni
 ya barabara wakishirikiana na watu wengine waliokua wakishabikia wakati
 wakiendelea na zoezi la kuwaondoa wafanya biashara wadogowadogo katika 
maeneo yasiyo ruhusiwa haswa kwenye hifadhi ya barabara ya mwanza kwenda
 shinyanga.
Aidha,
 Msangi amesema katika harakati za kudhibiti vurugu hizo askari 
walifanikiwa kuwakamata watu tisa ambao inadaiwa kuwa walikuwa 
wakihusika katika vurugu hizo kwa ajili ya mahojiano na uchunguzi 
utakapokamilika, watafikishwa mahakamani.
Majeruhi wote wapo hospitali ya mkoa ya Sekou Toure wakiendelea kupatiwa matibabu na hali zao inaendelea vizuri.

Post a Comment