Bw Trump anaongoza kwa wajumbe chama cha Republican kufikia sasa
Mgombea urais
anayeongoza katika chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump
amechukua hatua ya kushangaza akijaribu kuimarisha uhusiano uliodorora
kati yake na wakuu wa chama hicho.
Mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York ametembelea Kamati Kuu ya Taifa ya Republican.
Amechukua hatua
hiyo siku moja baada ya kuwakera viongozi hao kwa kusema kwamba hatatii
makubaliano ya kuunga mkono mgombea mwengine, iwapo yeye mwenyewe
hatashinda uteuzi wa chama hicho.
Bw Trump, anayeongoza kwa
wajumbe kwa sasa, amekosoa kile anachosema ni juhudi zisizo za
kidemokrasia za kutaka kumpkonya ushindi katika mkutano mkuu wa
kuidhinisha mgombea mjini Cleveland mwezi Julai.
Post a Comment