Maelfu ya Wakenya
kutoka maeneo tofauti nchini siku ya Jumamosi walikongamana katika chuo
kikuu cha Garissa ili kuadhimisha mwaka mmoja tangu shambulio baya la
kigaidi lililowauawa watu 148 wengi wao wakiwa wanafunzi.
Viongozi wa eneo hilo wakiongozwa na mbunge wa eneo hilo pamoja na kiongozi wa walio wengi bungeni Adan Duale walishiriki katika mbio hizo za kilomita 5.
Waandalizi wanasema kuwa mbio hizo zililenga kuleta uwiano kati ya Wakenya kufuatia shambulio hilo.



Post a Comment