0

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL)
 Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), imetoa tuzo ya Muonjaji Bora wa Bia kutoka barani Afrika.
 
Tuzo hiyo ilitolea katika shindano la kuonja vinywaji hicho lililoandaliwa na kampuni ya SabMiller na kushirikisha wafanyakazi wake wenye utaalam wa kuonja vinywaji kutoka katika viwanda vyake vilivyopo sehemu mbalimbali duniani.
 
Aliyeibuka mshindi wa tuzo hiyo ni Rebecca Semoka, kutoka Kiwanda cha Ilala jijini Dar es Salaam ambaye amekuwa muonjaji bora wa bia kutoka barani Afrika katika shindano ambalo hufanyika kila mwaka chini ya usimamizi wa kampuni ya kimataifa Aroxa inayoshughulika na usimamizi wa ubora wa bidhaa zinazozalishwa viwandani.
 
Mwaka huu shindano hilo lilijumuisha washindani kutoka mabara ya Afrika, Ulaya, Asia, Latin America na Amerika ya Kaskazini na hivyo Rebecca kuibuka mshindi kutoka Bara la Afrika.
 
Akizungumzia ya ushindi huo, alisema kuwa unatokana na elimu yake, mafunzo na mazoezi mbalimbali ambayo amekuwa akiyapata katika kampuni anayofanyia kazi ya TBL Group.

Post a Comment

 
Top