Zaidi ya watu 77 wamefariki katika tetemeko la kubwa ardhi kuwahi kukumbwa Ecuador katika kipindi cha zaidi ya mwongo mmoja .
Maafisa katika kituo cha Marekani cha utafiti wa kijiologia wamesema tetemeko hilo la ardhi lilikuwa la kiwango cha 7.8 kwenye vipimo vya Richter.
Taarifa katika mitandao ya kijamii nchini humo zaelezea jinsi mapaa ya majengo na hata baadhi ya madaraja na vivukio vya watembea miguu vilivyoporomoka kutokana na tetemeko hilo.
Awali Kituo cha kutoa onyo la uwezeano wa kutokea mafuriko, Pacific Tsunami Warning Centre kimesema huenda kukawa na mawimbi makali yatakayoweza kufikia maeneo yaliyokilomita 300 kutoka mahali tetemeko hilo lilipotokea.



Post a Comment