Rais wa Tanzania
John Magufuli amependekeza daraja mpya la Kigamboni lipewe jina la
mwanzilishi wa taifa hilo Mwalimu Julius Nyerere.
Daraja la Kigamboni lilianza kutumika tarehe 16 Aprili, 2016 na lina urefu wa mita 680 na barabara unganishi upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilomita 2.5.
Ujenzi wake ulifanywa na kampuni ya China Railway 15 Group ikishirikiana na kampuni ya China Bridge Engineering Group.
Daraja hilo ndilo la kwanza la kubeba uzito wa barabara kwa kutumia nyaya Afrika Mashariki na la tatu Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara bila kuhesabu Afrika Kusini.
Linamilikiwa na serikali ya Tanzania na Hazina ya Malipo ya Uzeeni (NSSF) kwa 40% na 60% mtawalia na litachukua nafasi ya feri ya MV Magogoni.
Ujenzi wa daraja hilo, ambao uligharimu dola 128 milioni za Kimarekani, ulianza mwaka 2012.
Post a Comment