Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Mhe. Dkt.  John Pombe Magufuli, leo
 tarehe 02 Machi, 2017 ameanza ziara ya kikazi ya siku 4 katika Mikoa ya
 Pwani, Lindi na Mtwara.
Katika
 ziara hiyo Mhe. Rais Magufuli atafungua miradi mbalimbali ya maendeleo 
na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.
Leo
 asubuhi Mhe. Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi la kiwanda cha 
kutengeneza vigae (Tiles) cha Tanzania Goodwill Ceramic Tiles Ltd. 
kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani na baadaye ataelekea Mkoani Lindi.
Kesho
 tarehe 03 Machi, 2017 Mhe. Rais Magufuli ataendelea na ziara yake 
Mkoani Lindi na keshokutwa tarehe 04 Machi, 2017 atafanya ziara yake 
Mkoani Mtwara.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
02 Machi, 2017

Post a Comment