Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Pwani limemkamata mmoja wa 
wamiliki wa eneo la maegesho ya magari la White Star, Munira Mbowe 
akidaiwa kujiunganishia umeme kinyume cha sheria. 
Mbowe ambaye 
ni mmiliki wa eneo hilo lililopo Kiluvya kwa Komba nje kidogo ya Jiji la
 Dar es Salaam, alikamatwa jana baada ya kufanyika msako wa kushtukiza 
kwa watu wanaodaiwa kujiunganishia umeme kinyume cha sheria. 
Inadaiwa kuwa Mbowe amelisababishia shirika hilo hasara ya Sh50 milioni. 
Akizungumza
 kwenye eneo hilo, Ofisa Usalama wa Tanesco Mkoa wa Pwani, Henry 
Byarugaba alidai kuwa baada ya kufanya ukaguzi waligundua umeme uliokuwa
 ukitumika katika eneo hilo haukuunganishwa na Tanesco. 
“Tumekuwa
 tukibuni mbinu mpya kila kukicha ya kuwatia mbaroni wateja wetu 
wanaotuhujumu na leo (jana), tumembana huyu anayedaiwa ni mmiliki wa 
yard hii ya White Star baada ya kukuta anatumia umeme wa wizi 
uliounganishwa katika njia tatu,” alidai Byarugaba. 
Alisema tayari wameshamfikisha Kituo cha Polisi Kibaha na hatua zingine za kisheria zinaendelea kuchukuliwa. 
Hata
 hivyo, alidai kuwa hiyo siyo mara ya kwanza kwa Mbowe kukamatwa kwa 
kosa hilo. Alidai mwaka jana Tanesco ilipofanya msako, ilimkamata akiwa 
amejiunganishia umeme na alichukuliwa hatua za kisheria. 
Alipoulizwa  kama tuhuma hizo zina ukweli, Mbowe alijitetea kuwa 
hajui ni nani aliyemuunganishia njia hizo tatu za umeme kwa sababu mara 
nyingi hufanya shughuli zake jijini Dar es Salaam, mara chache hufika 
kwenye yard hiyo kufanya kazi zingine ambazo ni chache. 
“Ni 
kweli tumekutwa na kosa la kuiba umeme, lakini jamani nataka niwaeleze 
kuwa mimi sihusiki na kingine, nawaomba msinitoe kwenye vyombo vya 
habari, haya ni maisha tu, sio vizuri kunitoa jamani mimi sihusiki 
kabisa katika wizi huu,” alijitetea Mbowe. 
Kaimu Meneja wa 
Taneso Mkoa wa Pwani, Selemani Mgwila alisema kitendo alichokifanya 
mteja wao huyo ni kosa kwani umeme waliokuwa wanautumia umesababisha 
upotevu wa mapato makubwa ya shirika. 
“Tunalalamika kila siku 
mpaka shirika linaonekana halifanyi kazi kwa sababu ya hawa watu 
wachache, safari hii lazima sheria ichukue mkondo wake,” alisema. 
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Pwani limemkamata mmoja wa 
wamiliki wa eneo la maegesho ya magari la White Star, Munira Mbowe 
akidaiwa kujiunganishia umeme kinyume cha sheria. 
Mbowe ambaye 
ni mmiliki wa eneo hilo lililopo Kiluvya kwa Komba nje kidogo ya Jiji la
 Dar es Salaam, alikamatwa jana baada ya kufanyika msako wa kushtukiza 
kwa watu wanaodaiwa kujiunganishia umeme kinyume cha sheria. 
Inadaiwa kuwa Mbowe amelisababishia shirika hilo hasara ya Sh50 milioni. 
Akizungumza
 kwenye eneo hilo, Ofisa Usalama wa Tanesco Mkoa wa Pwani, Henry 
Byarugaba alidai kuwa baada ya kufanya ukaguzi waligundua umeme uliokuwa
 ukitumika katika eneo hilo haukuunganishwa na Tanesco. 
“Tumekuwa
 tukibuni mbinu mpya kila kukicha ya kuwatia mbaroni wateja wetu 
wanaotuhujumu na leo (jana), tumembana huyu anayedaiwa ni mmiliki wa 
yard hii ya White Star baada ya kukuta anatumia umeme wa wizi 
uliounganishwa katika njia tatu,” alidai Byarugaba. 
Alisema tayari wameshamfikisha Kituo cha Polisi Kibaha na hatua zingine za kisheria zinaendelea kuchukuliwa. 
Hata
 hivyo, alidai kuwa hiyo siyo mara ya kwanza kwa Mbowe kukamatwa kwa 
kosa hilo. Alidai mwaka jana Tanesco ilipofanya msako, ilimkamata akiwa 
amejiunganishia umeme na alichukuliwa hatua za kisheria. 
Alipoulizwa  kama tuhuma hizo zina ukweli, Mbowe alijitetea kuwa 
hajui ni nani aliyemuunganishia njia hizo tatu za umeme kwa sababu mara 
nyingi hufanya shughuli zake jijini Dar es Salaam, mara chache hufika 
kwenye yard hiyo kufanya kazi zingine ambazo ni chache. 
“Ni 
kweli tumekutwa na kosa la kuiba umeme, lakini jamani nataka niwaeleze 
kuwa mimi sihusiki na kingine, nawaomba msinitoe kwenye vyombo vya 
habari, haya ni maisha tu, sio vizuri kunitoa jamani mimi sihusiki 
kabisa katika wizi huu,” alijitetea Mbowe. 
Kaimu Meneja wa 
Taneso Mkoa wa Pwani, Selemani Mgwila alisema kitendo alichokifanya 
mteja wao huyo ni kosa kwani umeme waliokuwa wanautumia umesababisha 
upotevu wa mapato makubwa ya shirika. 
“Tunalalamika kila siku 
mpaka shirika linaonekana halifanyi kazi kwa sababu ya hawa watu 
wachache, safari hii lazima sheria ichukue mkondo wake,” alisema. 

Post a Comment