Maafisa wa Serikali ya Canada
wamesema kuwa moto mkubwa, hatari na usioeleweka unatazamiwa kuvuka
mpaka wa Mkoa masaa machache yajayo.
Wazima moto wanatarajia kuwa moto huo kuvuka maeneo yanayochimbuwa mafuta Kaskazini mwa Fort McMurray.
Maafisa
hao wana hofu kuwa upepo huenda ukachochea moto huo na wakasema kuwa
mvua kubwa isipotokea moto huo utateketea kwa miezi kadhaa. Wazima moto wanatarajia kuwa moto huo kuvuka maeneo yanayochimbuwa mafuta
Mwandishi wa habari wa BBC ambaye ametembelea kambi
kadhaa za muda ambazo zinakaliwa na walioondolewa makwao anasema kuwa
wamepewa magunia ya vyakula, nguo na vifaa vya watoto kuchezea.
Post a Comment