Mwanamuziki mmoja kutoka Uingereza ameahirisha tamasha yake ya muziki visiwa vya Caribbean baada ya mbwa wake kuugua.
Aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kwamba aliahirisha tamasha ya Jumamosi kisiwa cha Barbados na Jumanne kisiwa cha Trinidad baada ya mbwa wake kuanza kuvuja damu.
“Najua linaonekana kama jambo la kushangaza lakini kwangu mbwa huyu ni kila kitu,” aliongeza.
“Nawaahidi nitarejea, lakini kwa sasa Missy yuko mbele ya mambo mengine yote,” aliandika.
Amesema anatumai kufanya onesho nchini Venezuela tarehe 21 Aprili mambo yakiwa sawa.
Post a Comment