Ilipoishia sehemu ya pili ( kama hukuisoma bofya hapa)
...Baada
 ya kukamilisha yote hayo Madam Mbeshi akasogeza kiti chake karibu na 
meza kisha akaketi halafu akaanza kusogeza vitu vilivyokuwepo mezani 
pale lakini ghafla akakutana na karatasi chafuchafu mezani kwake lakini 
ilikuwa na maandishi. 
Akashtuka
 kidogo halafu akaichukua ili aisome vizuri. Mwalimu Mbeshi hakutaka 
kuamini kile alichokiona, akataharuki kwa hofu na mshangao....
 Sehemu ya pili
...Mwalimu
 Mbeshi aliposoma ujumbe ule kutoka kwenye ile karatasi chafuchafu 
alizidi kuchanganyikiwa sana, mapigo ya moyo yalimwenda kasi kama gari 
iliyokata breki ikiwa mlimani. akarudia tena na tena ujumbe ule 
uliosomeka "POLE SANA MWALIMU KWA MASWAHIBU YALIYOKUKUTA SHULENI KWAKO..
 MIMI DOREEN MBWANA NIMEFANYA YOTE HAYO! PIA MUDA WA KIFO CHAKO U KARIBU
 KWANI UMESOMA UJUMBE WA MWANAFUNZI MCHAWI"
Jasho
 jembamba lilimtiririka mwanamama yule bila kuelewa afanye nini. Akataka
 kulitupa chini karatasi lile lakini ghafla akaona karatasi lile 
limebadilika ghafla, sio karatasi tena bali kitu kama ngozi ya binadamu 
iliyooza sana huku ikitoa harufu mbaya ikiwa imeambatana na funza wengi 
wakitembea tembea. 
Madam
 Mbeshi alihisi kinyaa sana huku woga ukiwa umemtawala kupita kiasi 
kwani katika maisha yake hakuwahi kushuhudia mauzauza ya namna ile hats 
Mara moja. Alitamani akimbie lakini miguu ilikuwa imeganda kama msumari 
kwenye sumaku. 
Mbeshi
 alihangaika sana na wale funza mkononi mwake kwani walizidi kumpanda 
mwilini kwa kasi na kumtia ghasia. Machozi yalimtoka mwalimu mbeshi 
lakini kila tone lililodondoka lilikuwa damu. 
Hofu
 ikamzidia sana, hakuwa na tumaini la kusalimika tena kwani kwa hatua 
aliyofikia ilitisha sana. Na yote hayo yalisababishwa na binti Doreen 
Mbwana.
Ghafla
 mlango wa ofisi ya mwalimu Mbeshi uligongwa lakini Mbeshi hakuwa hata 
na uwezo wa kuzungumza chochote. Mlango uligongwa sana lakini Mbeshi 
hakuweza kuufungua ingawa alitamani yule aliyegonga mlango aingie ili 
iwe ahueni kwake lakini ilishindikana. 
Kila
 aliponyanyua kinywa ulimi ulikuwa mzito na hakuweza kuzungumza chochote
 ikambidi atulie kimya akiugulia mateso yake yalimzonga ndani ya muda 
mfupi tu.
Post a Comment