Hatima
 ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema (Chadema), 
itajulikana Ijumaa wiki hii baada ya shauri hilo kurudishwa Mahakama Kuu
 Kanda ya Arusha kwa utekelezaji wa uamuzi wa Mahakama ya Rufaa.
Hatua
 hiyo imekuja baafa ya jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa 
Tanzania kufuta rufaa mbili za Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), dhidi ya  
mbunge huyo juzi mjini hapa.
Mmoja
 wa mawakili anaomtetea mbunge huyo, Adam Jabir, alisema shauri hilo 
litaamuliwa Machi 3, mwaka huu mbele ya Jaji Salma Maghimbi kutokana na 
rufaa ya Jamhuri namba 135 ya mwaka jana, inayopinga uamuzi wa Novemba 
11, mwaka jana wa Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Desderi 
Kamugisha kumpa Lema haki ya dhamana.
Novemba
 11 mwaka jana, Wakili Mwandamizi wa Serikali Paul Kadushi, alisimama 
wakati hakimu huyo akijiandaa kuandika masharti ya dhamana na kuieleza 
mahakama hiyo kuwa wameshasajili notisi ya kusudio la kukata rufaa 
Mahakama Kuu wakipinga uamuzi wa hakimu huyo kumpa Lema dhamana.
Hata hivyo,uamuzi huo wa dhamana haukuweza kutekelezwa kwa sababu ya nia ya kukata rufaa waliyoitoa mawakili hao wa Serikali.
Hakimu
 Kamugisha alishindwa kuendelea na mahsarti ya dhamana kwa mshitakiwa 
huyo ambapo,alikubaliana na upande wa Jamhuri na kusema kuwa notisi ina 
hadhi sawa na maombi ya rufaa yaliyowasilishwa Mahakama Kuu hivyo 
mwenendo na uamuzi wake utasimama mpaka uamuzi utakapotolewa na Mahakama
 Kuu.
Januari
 4 mwaka huu, Jaji Maghimbi alitarajiwa kusikiliza na kutoa uamuzi 
kuhusiana na dhamana ya Lema ila ilikwama baada ya  mawakili wa Serikali
 kukata Rufaa Mahakama ya Rufaa Tanzania,kupinga Jaji huyo  kusikiliza 
rufaa yao wenyewe.
Jaji
 Magimbi alitarajiwa kutoa uamuzi juu ya rufaa iliyowasilishwa na upande
 wa Jamhuri wakipinga Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kumpa Lema haki ya
 dhamana.
Uamuzi
 huo ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu na wakazi wengi wa jiji la Arusha,hasa
 ikizingatiwa mbunge huyo anashikiliwa katika mahabusu ya Gereza Kuu la 
Kisongo kwa zaidi ya miezi mitatu,tangu akamatwe na polisi nje ya 
viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Novemba 2, mwaka jana.
Aidha
 uamuzi huo ulikuwa unatarajiwa kutoa tafsiri ya kisheria ya notisi ya 
nia ya kukata rufaa iliyowasilishwa na na mawakili hao wa Jamhuri,notisi
 iliyosababisha Mahakama hiyo ya Hakimu Mkazi kutokuendelea na hatua ya 
kuweka masharti ya dhamana.
Akiahirisha
 uamuzi huo mahakamani hapo,Jaji huyo alisema kuwa mikono yake imefungwa
 na hawezi kusikiliza na kutoa uamuzi  kutokana na mawakili wa 
Serikali,kusajili nia ya kusudio la kukata rufaa Desemba 30 mwaka 
jana,katika Masijala ya Mahakama ya Rufaa Tanzania iliyopo mkoani hapa, 
kupinga asisikilize rufaa hiyo.
Awali
 kabla ya mawakili wa serikali kukata rufaa Mahakama ya Rufaa Tanzania 
kupinga kusikilizwa kwa rufaa yao Mahakama Kuu, Jaji Maghimbi,aliwataka 
mawakili wa Jamhuri  kuwasilisha hoja zao za rufaa Disemba 29,huku 
mawakili wa Lema wakitakiwa kujibu hoja hizo Disemba 30 kabla ya 
mahakama hiyo kutoa uamuzi wa rufaa hiyo jana.
Lema
 anakabiliwa na kesi mbili za uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli,
 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kesi namba 440 na 441.

Post a Comment