Jeshi la Congo-Brazzaville limeshambulia kwa mabomu vijiji vilivyoko Kusini mwa Poole na kusababisha maafa makubwa
Makanisa shule na hata zahanati za afya katika eneo la Poole lililoko Kusini mwa Congo Brazzaville zililengwa.
Walioshuhudia wanasema kuwa helikopta za kijeshi zilishambulia vijiji vya Vindza kwa zaidi ya mabomu 30.
Inadaiwa kuwa nyumba iliyolengwa ilikuwa makao ya Frederic Ntumi ambaye alikuwa akihudumu kama kiongozi wa kidini kijijini humo.

Mashambulizi hayo yanadaiwa kutekelezwa na jeshi Aprili tarehe 5 siku moja tu baada ya mashambulizi kutokea katika mji mkuu Brazzaville.
Waasi hao wanadaiwa kushambulia kambi ya kijeshi pamoja na vituo vinne vya polisi.
Wakati huo Ninja walikuwa ni wafuasi wa waziri mkuu wa zamani Bernard Kolelas ambaye ni babake mgombea wa urais Guy-Brice Parfait Kolelas, aliyejizolea asilimia 15 % ya kura katika uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi Machi mwaka huu.
Post a Comment